CCM Moshi mjini yampongeza Rais Dkt.Samia Suluhu yataja mafanikio

 Safina Sarwatt,Moshi,

CHAMA cha Mapinduzi (CCM ) wilaya ya Moshi M
jini  Mkoani wa Kilimanjaro, kimeunga mkono maamuzi ya mkutano mkuu wa  CCM Taifa  uliofanyikika Tarehe 18-19/01/2025, kwa kuwapitisha wagombea wa Urais, Dkt.Samia Suluhu Hassan  kuwa  mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Emmanuel  Nchimbi  kuwa Mgombea mwenza wa urais pamoja na Dkt.Hussen  Ally Mwinyi  kuwa Mgombea urais wa Zanzibar.

 

 Mkutano huo ulifanyika kwenye soko  la nafaka la  Mbuyuni  Mjini Moshi na

kuhudhuriwa na wanachama wa chama hicho,wafanyabiashara wa soko hilo pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali.

 





Akizungumza katika mkutano huo mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MNEC) Seleman Mfinanga alisema kuwa  katika uongozi wa rais Dkt Samia Suluhu Hasan mkoa huo umepokea fedha nyingi kwa ajili mirandi mbalimbali ya maendeleo.

 

Alisema kuwa ndani ya miaka minne ya uongozi wa Dkt.Samia Suluhu Hasan mkoa wa Kilimanjaro ulipokea fedha zaidi ya billion 956.63 kwa ajili ya miradi ya maendeleo 1,360.

 






“Sekta ya afya billion 117,Elimu billion 149.64,Ujenzi billion 125.46,Maji billion 370.87,Nishati billion 67.2,wateja waliounganishiwa umeme na Tanesco 98,9,wateja waliounganishwa huduma ya umeme kupitia Rea 5352,Utalii billion 4.62,Kilimo na Mifungo billion 28.36,”alisema Mfinanga.

 

 

 

Mfinanga aliwashukuru wananchi  kwa kukipigia kura chama cha mapinduzi(CCM)katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika mwaka jana na  kuwaomba kuendelea kukiamini na kumpa kura nyingi Rais Dkt Samia Suluhu katika uchaguzi mkuu ujao mwezi Oktomba ,

 

 




Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu alisema serikali tayari imetoa fedha Zaidi ya billion  489 kwa ajili ya upanuzi wa  barabara kuanzia eneo la Holili wilayani Rombo  hadi  Daraja laa kikavu wilaya ya Hai.



 

Alisema  Moshi mjini itajengwa km 15 za barabara 4 pamoja na ujenzi wa daraja mpya la kikavu na kwamba daraja la zamani halitavunjwa  nabadala yake litatumiwa na wananchi.

 

Babu  aliwakata wananchi na wafanyabiashara katika soko la Mbuyuni kutumia soko hilo ambalo limejengwa miondombuni ya kisasa bila ubaguzi na kila mmoja kurudi katika nafasi yake kwa utaratibu wa awali.

 




Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Moshi Zuberi Kidumo alisema manispaa hiyo itaweka utaratibu wa wafanyabishara wa karoti  kwa kuwapangia eneo lenye miundombinu rafiki kwa ajili ya kuosha karo zao kabla kupelekwa sokoni.

 

 

mwisho….

Post a Comment

0 Comments