Safina Sarwatt,Moshi,
MKUU wa wilaya Moshi Godfery Mzava ametangaza vita dhidi ya wanaume wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja(MASHOGA)pamoja na wanawake wanaojihusisha na vitedo vya usagaji.
Ametangaza vita hivyo hivi karibuni kwenye kikao cha bazara la kikanuni la umoja wa wanawake wa chama cha Mpinduzi CCM (UWT)wilaya Moshi mjini mkoani Kilimanjaro.
“Kuna changamoto kubwa sana hapa moshi vijana wetu kuangukia katika wimbi kumbwa la unywaji wa pombe haramu gongo pamoja na vitendo vya usagaji na ushoga na kushindwa kutoa mchangao wao katika shughuli za maendeleo,”
Alisema Changamoto ya vitendo vya ushonga kwenye wilaya moshi ni kubwa lakini watu wanashindwa kuvisemea kutokana na kuona aibu.
Alisema serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan haikubaliane n'a vitendo hivyo ambavyo vinadhalilisha utu na kwamba lazima Sheria ichukue mkondo wake kwa watu wanaojihusisha na vitedo hivyo.
"Serikali yenu ya awamu ya sita chini ya jemedali wake Dkt.Samia Suluhu Hassan haitafumbia macho vitendo hivyo,hatuwezi kuwa na vijana ambao muda wote wamelewa na kufanya vitendo vya kudhalilisha utu",alisema.
Alitumia kikao hicho kuwaasa kina mama kuwaonya vijana ambao wanaenda kinyume na maadili na kwamba serikali haiwezi kuwa na kundi kubwa la vijana tegemezi ambao hawawezi kufanyakazi kutokana na kujikita kwenye ulevi.
Aliitaka jumuiya hiyo ya wanawake ya CCM kuwa kuwa mstari wa mbele kusaidia malezi ya vijana kwa kuwaasa waachane na vitendo vya ushonga,usagaji na ulevi pamoja na matumzi ya dawa za kulevya.
"Naomba niwaambia kwamba katika vitendi hivyo na mimi ninaomba niwe sadaka kupambana na vita hivyo vya usagaji na ushonga kwa kweli hatuwezi kufumbia macho vitendo hivyo",alionya .
“Najua ni jambo nzito, watu wenye fedha wanafanya vitendo hivyo kwa siri na kuwarubuni vijana lakini kwa sababu sheria zipo ,niwaombe mama zangu muwe sehemu ya mapambano haya",alisema.
Aliomba ushirikiono katika mapambano dhidi ya vitendo hivyo hata kama tatizo hilo halitamalizwa ndani ya muda mfupi lakini lazima jamii ione kwamba serikali haikubaliani na jambo hilo ambalo alisema haliendani na maadili ya kiafrika.
Katibu wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro,Mecy Mollel alisema kama chama wako tayari kupambana na vietendo hivyo ya ushoga ambavyo alisema vinadhalilisha utu na kushusha heshima ya watoto wa kiume.
Alisema kuwa vijana wengi wamejiingiza katika vitendo vya usagaji na ushonga kutokana na matumizi ya dawa za kulevya na unywa wa pombe haramu.
Alisema kuwa chama hicho kinahitaji wapiga kura lakini pia kinahitaji nguvu kazi ya taifa yenye maadili mema na uadhlifu.
Alisema kuwa vitendo hivyo vimesababisha watu kutokuwa na uwezo wa kuzaliana hivyo baadhi ya shule kukokasa wanafunzi.
Naye mbunge wa jimbo la Moshi mjini Priscus Tarimo alisema kuwa serikali ya awamu ya sita chini ya Dkt.Samia Suluhu Hassana imeleta fedha nyingi katika manispaa ya Moshi zikiwamo za ujenzi wa uwanja ndogo wa ndege wa Moshi na kwamba hakuna sababu ya Rais Samia kukosa kura za kutosha katika uchaguzi mkuu mwezi Oktoba 2025.
Alisema kuwa serikali imetekeleza miradi mingi ya maendeleo hakuna haja ya kujibishana na mtu wala kuchambua na kutukana na watu na kiwataka wanaCCM tujivunie hilo.
Alitaja maeneo ambayo fedha hizo zitumika ikiwa ni pamoja na jengo la Mama na Mtoto katika Hospital ya rufaa ya mkoa ya mawenziuboreshwaji was vifaa vya afya .
Maeneo mengine ni kuboreshwa kwa upatikana wa maji safi na salama kwa asilimia100 ,huduma ya meme ambako wananchi wengi wameunganishwa kwenye huduma hiyo wananchi huku serikali ikiboresha elimu kwa shule nyingi kuwa na vyumba vingi vya madarasa yakiwamo yaliyojengwa katika viwango vya ubora unaotakiwa.
mwisho
0 Comments