Zara Tours yaanzisha kampeni ya “TWENDE ZETU SEERENGETI”

 

Safina Sarwatt,Serengeti,

 


Kampuni ya wakala wa Utalii nchini ya Zara Tanzania  Adventures.imeanzisha kampeni ya kila  mwezi Desemba kuhamasisha Watanzania kwenda kutembelea vivuto vya utalii  katika Hifadhi ya taifa ya Serengeti itwayo “TWENDE ZETU SERENGETI

 

Lengo la kampeni hiyo ni katika jitihada za  kuunga mkono juhudi za Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan katika kukuza utalii wa ndani na kuongeza ajira kwa vijana.

 




Hii ni kampeni ya pili katika kuhamasisha watanzania kutembelea vivutio vya utalii baada ya ili ya awali ya “TENDE ZETU KILELLENI”ambayo ni mahususi katika kusherehekea siku ya uhuru wa Tangaznyika ambayo hufanyika kila Desemba 5 kila mwaka.

Ni tukio ambalo huwakutanisha watanzania wengi katika kupanda mlima Kilimanjaro na kufika kilele cha Uhuru Desemba 9 mbayo ndiyo siku ya Uhuru.

 




Kampeni ya “TWENDE ZETU SERENGETI,”sasa imeingia msimu wake wa tatu tangu kuanzishwa kampeni inayoonekana kuleta mwamko mkubwa kwa Watanzania kutokana na kujitokeza kwa wingi kutembelea Hifadhi ya Taifa ya  Serengeti .

 

Mkurugenzi wa kampuni Zara Tanzania Adventures ,Zainab Ansell mwanzilishi wa kampeni hiyo anasema kampeni hiyo itakuwa endelevu ikiwa ni mkakati wa kuhasisha watanzaia kujenga utamaduni wa kutembelea vivutio vya utalii.

Kwa upande wake Rafael Masaki kutoka idara ya  Masoko ya kampuni hiyo ya Zara anasema kampeni hiyo inalenga kuchochea utalii wa ndani pamoja na kutangaza vivutio vya utalii vilivopo nchini.

 Mwaka  jana kampuni hiyo ilitoa ofa kwa watanzania kutembelea hifadhi za Taifa za Tarangire,Manyara,Serengeti pamoja na Mamlaka ya hifadhi ya Ngorogoro  kwa gharama nafuu ya sh,850,000 ikihusisha chakula na malazi kwa siku mbili katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti .

 





Raphael aansema kuwa zara imekuwa ikitoa michango mikubwa katika kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa wageni wote wanatembelea Serengeti kwa gharama nafuu ya shilingi 850,000/= mtu moja na watoto miaka (14) 450,000/= kwa siku mbili ndani ya hifadhi ya Serengeti.

 

Anasema kuwa idadi ya watalii wanaojitokeza kushiriki kampeni hiyo ya “twende zetu Serengeti” imeongezeka  ikilinganishwa na mwaka 2023 hii ni kutokana  na huduma nzuri inayotolewa na kampuni hiyo.

 

Anasema kampuni hiyo imeona umuhimu wa  kutangaza utalii kupitia kampeni hiyo ikiwa ni mikakati ya kuhakikisha wanaunga mkono juhudi za Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ya kutangaza utalii wa ndani ili kuongeza mapato ya taifa na soko la uhakika la utalii.

 

 

Mbali na kampeni hiyo ,Zara Tours wamekuja na progamu mpya ya kwende Serengeti siku ya wapendano kila mwaka mwezi wa nne na kwa mwaka wanafanya kampeni ya kupeleka wageni mara tatu .

 

Alisema kampeni hiyo itaweza kuleta hamasa kubwa kwa watanzania pamoja na  kuchochea uchumi wa nchi  kupitia sekta ya utalii.

 

 

Joseph Chitinka mmoja wa watalii wa ndani na  mkazi wa Dodoma waliotembelea vivutio vya utalii kupitia kampeni hiyo,alitoa wito kwa watanzania kuthamini rasilimali  za ndani ikiwamo  kuzitangaza.

 

“Nitoe wito kwa watanzania wenzangu kujenga utamaduni wa   kutembelee vivutio  vya utalii kwani kwa kufanya hivyo itasaidia kuchochea uchumi wa taifa na  uchumi wa mtu mmoja mmoja”.alisema.

 

anasema Rais Dkt.samia Suluhu Hassan  alishafungua milanga baadaya kuzindu giamu ya Royal Tour  na kuwataka watanznaia kuunga mkono jitihada hizo za rais  kwa kutembelea vivutio vya utalii na kukuza pato la Taifa.

 

“Lengo la rais kufungua kampeni yake kupitia filmu ya Royal  Tour ni kukuza soko la utalii wa ndani badala ya kutegemea watalii kutoka mataifa ya nje na hata  yakitokea majanga kama ilivyotokea UVICO 19 sekta hiyo isiyumbe na makampuni ya utalii yaendelee na kazi”.

 

Alisema watanzania wanapaswa kumwelewa Rais  Samia Suluhu Hassan kwani amekuwa na maono ya kuona mbali kwa kuanzisha Royal tour na kwamba watanzania wameyaona  matokea yake .

 

 

Kuongezeka kwa utalii wa ndani umefungua fursa kwa vijana wa kitazania na makapuni ya utalii kufanya kazi misimu yote ya mwaka.

 

Judith Ngowello anasema wamejifunza  mambo mengi na kupongeza ubunifu ulioanzishwa na kampuni ya Zara Tours kwa kuanzish kampeni ya “twende zetu Serengeti”kampei inayowalte watanzania pamoja .

 

“Jambo la kipekee na ambalo  halitafutika kwenye historia yetu ni  watoto wetu kujionea wanyama kwa macho  tofauti na awali ambako walikuwa wakiwaona kupitia luninga”

 

Zara tours ndiyo kampuni  pekee ambayo imejijengea uzoefu kwa Zaidi ya miaka 30 ikiwa na  uzoefu wa kuhudumia wageni wa ndani nan je ya nchi wakiwamo  watoto .

 

 

 Moureen Robert ni mmoja wa watoto waliotembelea hifadhi hizo na kujioa vivutio vya utalii.

 

Anasema  wamejifunza mengi na  mbali ya kuona wanyama wakubwa kama,tembo,simba,twiga,pundamilia,nyati,faru,chui,ngiri,duma,swala,viboko na ndege pia walifurahia  utalii huo kupitia kampeni hiyo ya “ twende zetu Serengeti”.

 

Anasema walizoea kuwaona wanyama hao kupitia vipindi vya   television lakini kupitia kampeni hiyo ya twende zetu Serengeti  wameshuhudia maajabu  na wamejifunza mengi.

Hifadhi ya taifa ya Serengeti ni moja ya Hifadhi Tano(Big Five}ambazo zimekuwa zikiingiza watalii wengi na kuliingizia taifa fedha za kigeni.

 

Katika mwaka wa fedha wa 2023/2024 watalii 1.451,176 walitembelea hifadhi za Taifa ikiwa ni takwimu zilizofikia mwenzi februari mwaka jana huku Serengeti ikiongoza kwa idadi kubwa ya wageni.

 

 

Mwisho…..

 

Post a Comment

0 Comments